KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Thursday, August 12, 2010

BEBE ATUA MAN UTD.


Klabu ya Manchester United imekamilisha usajili wamshambuliaji wa kimataifa toka nchini Ureno na klabu ya Vitoria de Guimaraes - Tiago Manuel Dias Correia Bebe.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na uongzoi wa klabu hiyo ya jijini Manchester zimeeleza kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 20 amesajiliwa baada ya kupita kwenye vipimo vya afya alivyofanyiwa siku mbili zilizopita.

Mshambuliaji huyo mwenye urefu wa futi 6 na nchi 3 amejiunga na klabu hiyo na mashetani wekundu kwa ada ya uhamisho wa paund million 7.4.

Kusajiliwa kwa Tiago Manuel Dias Correia Bebe kunaifanya klabu ya Man utd kufikisha idadi ya wachezaji watatu waliosajiliwa katika kipindi hiki ambapo mjiongoni mwa wachezaji hao ni Javier Hernandez Chacharito toka nchini Mexico pamoja na Christopher Lloyd Smalling.

No comments:

Post a Comment