KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, August 18, 2010

SPURS YAKWAMA.



Michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu wa mwaka 2010-11 hatua ya mtoano imendeelea tena usiklua wa kuamkia hii leo kwa michezo kadhaa kuchezwa katika viwanja tofauti.

Katika uwanja wa Wankdorf wenyeji BSC Young Boys wameanza vyema katika mchezo wa kwanza wa hatua ya mtoano baada ya kuibanjua Tottenham Hotspours mabao matatu kwa mawili.

Mabao ya BSC Young Boys katika mchezo huo yamefungwa na Senad Lulic 4, Henri Bienvenu 13, na Xavier Hochstrass 28 huku mabao ya Tottenham ya kufutia machozi yakifungwa na Sebastian Bassong 42 na Roman Pavlyuchenko 83.

Meneja wa klabu ya Tottenham Harry Redknapp amesema licha ya kupokea kichapo cha mabao matatu kwa mawili bado kwake ni faida kubwa katika mchezo wa marudiano utakaochezwa jijini London juma lijalo.

Rednapp amesema tofauti ya bao moja iliopo katika idadi ya mabao waliyofungwa bado anaamini wataifikia na kufanikisha safari ya kusonga mbele.


Michezo mingine ya michuano hiyo iliyochezwa jana ni pamoja na

Petrovski Stadium (20,000)
Zenit St Petersburg 1 - 0 AJ Auxerre

Valeri Lobanovski (16,000)
Dynamo Kiev 1 - 1 Ajax Amsterdam

Lerkendal (18,800)
Rosenborg 2 - 1 FC Copenhagen

AXA Arena (19,000)
Sparta Prague 0 - 2 MSK Zilina


Michuano hiyo ya ligi ya mabingwa barani ulaya iliyo kwenye hatua ya mtoano inaendelea tena hii leo huko

Estadio Municipal de Braga
Braga v Sevilla FC

St Jakob Park
FC Basel v Sheriff Tiraspol

FK Partizan Stadium
Partizan Belgrade v Anderlecht


Bullen-Arena
SV Salzburg v Hapoel Tel-Aviv


Weserstadion
Werder Bremen v Sampdoria

No comments:

Post a Comment