KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Tuesday, August 24, 2010

UKAME SASA BASI!!!!


Kiungo wa kimataifa toka nchini Urusi na klabu ya Arsenal Andrey Arshavin amesema baada ya The Gunners kumaliza misimu mitano bila kutwaa ubingwa wa michuano yoyote, wakati umewadia kwa klabu hiyo kufanya vyema.

Akitoa sababu za kuipa nafasi Arsenal msimu huu Andrey Arshavin amesema anaamini kikosi chao msimu huu kimepevuka kwa kiwango kikubwa hivyo ni jambo gumu sana kwao kumaliza pasipokua na ubingwa wa ligi.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29 ameongeza kuwa msimu uliopita walikaribia kufanya vizuri tena kwa kuzipa mshawasha klabu ya Chelsea pamoja na Man Utd na mwisho wa ligi walijikuta wakizidiwa point chache na klabu hizo ziliomaliza katika nafasi mbili za juu.

No comments:

Post a Comment