KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, August 8, 2011

Kwadwo Asamoah AJIENGUA KIKOSINI.


Kiungo Kwadwo Asamoah ameachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ghana kitakachocheza kesho.

Kwado ameondolewa kikosini kufuatia taarifa aliyoituma kutoka nchini Italia akiwa na klabu yake ya Udanise ambapo ameeleza kwamba amepatwa na maumivu wa kifundo cha mguu akiwa katika maandalizi ya msimu mpya wa ligi.

Hata hivyo wachezaji wengine walioitwa na kocha mkuu Goran Stevanovic kutoka nje ya bara la Afrika wameshawasili kambini na kesho wanatarajia kujumuyishwa kikosini.

Michezo mingine ya kimataifa ya kirafiki kwa bara la Afrika itachezwa siku ya jumatano ambapo;

Senegal v Morocco, Dakar

Africa Kusini v Burkina Faso - Johannesburg

Gabon v Guinea - Paris

Equatorial Guinea v Guinea-Bissau - Lisbon

Zimbabwe v Zambia - Harare

Tunisia v Mali - Monastir

Ivory Coast v Israel - Geneva

Botswana v Kenya - Gaborone

Liberia v Angola - Monrovia

Malta v jamuhuri ya Afrika ya kati - Malta

The Gambia v DR Congo - Banjul

No comments:

Post a Comment