KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Friday, September 30, 2011

King Kenny Dalglish AWAHUSIA MABEKI WAKE.

Meneja wa majogoo wa jiji Liverpool King Kenny Dalglish ameitaka safu ya ulinzi ya kikosi chake kufanya juhudui ambazo zitawawezesha kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kutoruhusu kufungwa katika mchezo wa ligi dhidi ya Everton utakaochezwa kesho huko Goodson Park.

King Kenny Dalglish ametoa wito huo kufuatia wachezaji wake kufanya vyema katika mchezo uliopita ambapo walifanikiwa kuchomoza na ushindi dhidi ya Wolves waliokubali kisago cha mabao mawili kwa moja.

Amesema endapo safu yake ya ulinzi itakua makini kuna uhakika wa kufanya vizuri hiyo kesho ambapo kutakua na upinzani wa hali ya juu kutokana na upinzani wa klabu hizo pale zinapokutana.

Hata hivyo sababu kubwa iliyopelekea King Kenny Dalglish kuwahimiza wachezaji wake wananaocheza nafasi ya ulizni ni kutotaka kurejesha tofauti kubwa ya mabao ya kufungwa na kufunga ambapo kwa sasa msimamo wa ligi unaonyesha Liverpool katika kipingele hicho hana bao analodaiwa.

Everton wao wataingia katika uwanja wao wa nyumbani hiyo kesho huku wakiwa na kumbu kumbu ya kupoteza mchezo uliopita ambapo walikubali kisago cha mabao mawili kwa sifuri kutoka kwa Man City waliokua nyumbani huko Etihad Stadium.

No comments:

Post a Comment