KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Friday, September 30, 2011

Titus Bramble AFUNGIWA.

Uongozi wa klabu ya Sunderland umetangaza kumsimamisha kwa muda, beki wa klabu hiyo Titus Bramble ambae anakabiliwa na tuhuma za ubakaji pamoja na kukutwa na dawa za kulevya.

Uongozi wa klabu hiyo ya Stadium Of Light, umemsimamisha beki huyo mwenye umri wa miaka 30, kwa kipindi ambacho hakikuwekwa wazi lakini taarifa zingine zinadai kwamba huenda akarejea kikosini mara baada ya kukamilika kwa kesi inayomkabili.

Adhabu hiyo pia inahusisha harakati za kufanya mazoezi na kikosi cha klabu ya Sunderland ambacho mwishoni mwa juma hili kutaendelea na mkakati ya kusaka point tatu muhimu katika ligi kuu ya soka nchini Uingereza mara baada ya kukubali kisago cha mabao mawili kwa moja kutoka kwa Norwich city mwanzoni mwa juma hili.

Titus Bramble alikamatwa na jeshi la polisi nchini Uingereza siku mbili zilizopita, na kufanyiwa mahojiano na askari wa jeshi hilo, lakini jana aliachiwa kwa dhamana.

No comments:

Post a Comment