KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, July 15, 2009

PAUND MILION 300 ZA MAN CITY HUENDA ZIKAPUNGUWA.

Imeelezwa kuwa zaidi ya paundi million 300 zimetengwa na klabu ya MANCHESTER CITY kwa ajili ya usajili huenda zikapunguwa pale kikosi cha klabu hiyo kitakaporejea toka nchini Afrika Kusini mwishoni mwa wiki hii.

Hatua hiyo imeelezwa kufuatia klabu hiyo kutuma offer ya paundi milioni 25 kwenye klabu ya Arsenal kwa lengo la kumsajili mshambuliaji wao wa kimataifa toka nchini Toga Emmanuel Adeboyor .

Adeboyor anataraji kusaini mkataba wa miaka mitano utakaomwezesha kuwepo huko Cit of Manchester na kulipwa mshahara wa paundi laki moja na elfu thelathini kwa juma.


Man city wameelekeza nguvu zao usajili kwa Adebayor baada ya kukatishwa tamaa na hatua ya kumsajili mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Cameroon na klabu ya Barcelona Samuel Etoo.
Iwapo Man City watafanikiwa kumsajili mshambuliaji huyo watakuwa wametumia jumla ya paundi milioni sitini halia mbayo huenda ikapunguza kiasi cha fedha za kumsajili nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza na klabu ya Chelsea John Terry iwapo uongozi wa klabu hiyo utafanikiwa katika hatua hiyo.

Kiasi kingine cha fedha kilichotengwa na Man City ni paundi milioni 40 kwa ajili ya Terry ambapo wamaahidi kumlipa mshahara wa paundi laki 2 na nusu kwa juma.

Mwezi uliopita mmiliki wa klabu hiyo Sheikh Mansour aliahidi kuwa tayari kukijenga kikosi cha klabu huyo hukua kitegemea ushirikiano mkubwa toka kwa watendaji wenzake klabuni hapo.

Tayari klabu hiyo imeshakamilisha usajili wa mshambulaiji wa kimataifa toka nchini Paraguay alietokea kwenye klabu ya Blackburn Rovers Roque Santa Cruz ambae atakuwa nalipwa mshahara wa paund elfu 80 kwa juma, kiasi ambacho ni mara mbili zaidi ya kiasa alichokuwa analipwa na klabu yake ya zamani.
Mchezaji mwingine aliesajiliwa klabuni hapo ni Gareth Barry ambae atakuwa nalipwa mshahara wa paund elfu 90,000 kwa juma.

No comments:

Post a Comment