KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Thursday, August 6, 2009

KWELI NG'OMBE WA MASKINI HAJIFUNGUI !!!!.


Kiungo wa klabu ya Arsenal Tomas Rosicky ataikosa michezo ya awali ya msimu ujao kufuatia ripoti ya daktari wa klabu hiyo kuonyesha kwamba kiungo huyo atakuwa nje kwa muda wa majuma sita.

Kiungo huyo wa kimataifa toka Jamuhuru ya Czech ndio kwanza alikuwa amerejea katika kikosi cha Arsen Wenger baada kuuguza majeraha yake ya nyonga na goti kwa muda wa miezi 18.

Kufuatia hatua hiyo Rosicky ataikosa michezo ya kufuzu kwa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani ulaya pamoja na michezo minne ya ligi kuu ya soka nchini Uingereza msimu ujao.

No comments:

Post a Comment