KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, July 20, 2009

MSIMAMO WA HUYU MZEE BALAA !!!!!!


Meneja huyo wa kimataifa toka nchini ufaransa amebainisha wazi kuwa anafahamu kwa sasa kila shabiki wa klabu ya Arsenal kwa sasa atakuwa na hamu ya kutaka kufahamu ni mchezaji yupi atakaesajiliwa klabuni hapo lakini kwake haoni sababu ya kuliharakisha jambo hilo.


Wenger amesema ukikitazama kikosi chake kwa sasa kuna washambuliaji walio mahiri kama Van Persie, Arshavin, Walcott, Bendtner pamoja na Eduardo huku Thomas Rosicky akitarajiwa kuwepo katika kikosi cha kwanza msimu ujao baada ya kupona majereha yake na mwishoni mwa juma lililopita alirejea katika mchezo wa kujipima nguvu ambao ulimazika kwa sare ya mbao mawili kwa mawili dhdi ya klabu ya Barnet.

Hata hivyo amesema atakuwa tayari kutumia ada ya uhamisho wa Adebayor iwapo atampata mchezaji alie na umakini mkubwa na mwenye uwezo wa kuisadia Arsenal katika michuano kadha wa kadha msimu ujao.

Katika hatua nyingine Arsene Wenger ameendelea kuweka wazi mapenzi yake ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Morroco na klabu ya Bordeaux ya nchini ufaransa Morouane Chamakh kwa kueleza kwamba bado ni chaguo lake la kwanza iwapo atalazinika kufanya usajili katika kipindi hiki.


No comments:

Post a Comment