KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, July 20, 2009

WIGAN YAENDELEA KUJIIMARISHA.


Klabu ya Wigan Athletic imekamilisha usajili mshambuliaji wa kimataifa toka Trinidad na Tobago, Jason Scotland kwa ada ya uhamisho wa paund million 2.

Jason Scotland amejiunga na klabu hiyo ya ligi kuu ya soka nchini Uingereza akitokea katika klabu yake ya daraja la kwanza nchini humo ya Swansea.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 30 amesaini mkataba na klabu yake hiyo mpya wa miaka miwili na amesema ana amini muda huo utamuwezesha kuisadia kwa hali na mali Wigan katika msimu mpya wa ligi kuu.

Jason Scotland ameongeza kuwa imekuwa kama ndoto kwake kujiunga na klabu hiyo na kucheza ligi kuu ambayo kila kukicha ilikuwa kama sehemu ya mawazo yake na alijitahidi sana kuisaidia klabu yake ya zamani ya Swansea ili nayo siku moja iweze kuchea ligi hiyo ikitokea ligi daraja la kwanza.

Msimu uliopita mshambuliaji huyo aliweza kuipachikiwa klabu yake ya Swansea mabao 24 na hatua hiyo yasemekana imekuwa chanzo cha benchi la ufundi la klabu yake ya sasa kuanza kumfuatilia mpka kufanikiwa kumsajili.


No comments:

Post a Comment