KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, July 22, 2009

NGOJA NGOJA YA ARSENE WENGER !!!!!!!!!


Klabu ya Olympic Lyon ya nchini Ufaransa imeingia kati taratibu za meneja wa klabu ya Arsenal Arsen Wenger za kutaka kumsajili mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Morocco na klabu ya Bordeaux Marouane Chamakh.


Olympic Lyon wametanmgaza hatua hiyo ambayo inadhihirisha kwamba wapo katika mawindo makali ya kutaka kumsajili chamakh.


Akitangaza taratibu za kuvutiwa na mshambuliaji huyo, raisi wa klabu ya Olympic Lyon, Jean-Michel Aulas amesema wamevuitiwa na uchezaji wa Chamakh ambae anapigiwa upatu wa kuziba pengo lililoachwa wazi na Karim Benzema alietimkia huko nchini Hispania katika klabu ya Real Madrid.


Amesema ana imani mshambuliji huyo hatokataa kujiunga nao kufuatia mazingira yaliopo sasa kuyazoea mbali na kutoka nje ya Ufaransa ambapo huko mazingira yatakuwa mageni kwake na itamchukuwa muda kuonyesha soka lake la kisawa sawa.


Ikumbukwe kuwa meneja wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger alivieleza vyombo vya habari kwamba, Chamakh ni chaguo lake la kwanza katika harakati zake za kumsaka mrithi wa nafasi ya Emmanuel Adebayor aliejiunga na Man City mwishoni mwa juma lililopita.

No comments:

Post a Comment