
Mfanyabiashara wa kimataifa toka Dubai Sulaiman Al Fahim amethibitishwa kuwa mwenyekiti mpya wa klabu ya Porthmouth ambayo ni miongoni mwa vilabu vitakavyoshiriki ligi kuu ya soka nchini Uingereza msimu ujao.
Al Fahim amethibitishwa kushikwa wadhifa huo baada ya kusikika kwa taarifa za fununu kwa muda wa majuma madhaa kwamba yu mbioni kuinunuwa klabu hiyo hali ambayo hii leo imetimia na kuwekwa hadharani kupitia vyombo vya habari.
Mfanyabiashara huyo amechukuwa madaraka ya kuwa boss wa klabu hiyo kutoka kwa Alexandre Gaydamak ambae alikuwa akiimiliki klabu hiyo kwa asilimi kubwa ya hisa hatua ambayo sasa inadhihirisha ni vipi klabu hiyo itaanza kuingia kwenye ushindani wa kisoka pamoja na kibiashara.
No comments:
Post a Comment