KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Tuesday, July 21, 2009

Sulaiman Al Fahim AFANIKIWA.


Mfanyabiashara wa kimataifa toka Dubai Sulaiman Al Fahim amethibitishwa kuwa mwenyekiti mpya wa klabu ya Porthmouth ambayo ni miongoni mwa vilabu vitakavyoshiriki ligi kuu ya soka nchini Uingereza msimu ujao.

Al Fahim amethibitishwa kushikwa wadhifa huo baada ya kusikika kwa taarifa za fununu kwa muda wa majuma madhaa kwamba yu mbioni kuinunuwa klabu hiyo hali ambayo hii leo imetimia na kuwekwa hadharani kupitia vyombo vya habari.

Mfanyabiashara huyo amechukuwa madaraka ya kuwa boss wa klabu hiyo kutoka kwa Alexandre Gaydamak ambae alikuwa akiimiliki klabu hiyo kwa asilimi kubwa ya hisa hatua ambayo sasa inadhihirisha ni vipi klabu hiyo itaanza kuingia kwenye ushindani wa kisoka pamoja na kibiashara.

No comments:

Post a Comment