KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, July 15, 2009

Stewart Downing anaswa!!!!!!


Klabu za MIDDLESBROUGH imekubali kumuuza winga wake wa kimataifa toka nchini Uingereza Stewart Downing kwa gharama ya paund million 12 ambazo zimetolewa kama ada ya uhamisho na klabu ya Aston Villa.


Makubaliano ya vilabu hivyo viwili yanamfanywa winga huyo mwenye umri wa miaka 24 kuondoka nyumbani kwao alipozaliwa na kutarajia kuanza maisha mapya huko Birmingham yalipo makao makuu ya klabu ya Aston Villa.


Hata hivyo kwa sasa Downing yu mbioni kurejea katika hali yake ya kawaida baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo katika mguu.

No comments:

Post a Comment