KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Thursday, July 16, 2009

SAFARI YA PETER CROUCH YAENDELEA.


MENEJA wa klabu ya Sunderland Steve Bruce amethibitisha kuwa angependa kumsajili mshambuliaji Peter Crouch licha ya kukiri bado hawajaafikiana na klabu ya Portsmouth kuhusu gharama za usajili wake.


Awali Crouch alihusishwa na taarifa za kutaka kujiunga na klabu ya Fulham, lakini meneja Steve Bruce ameendelea na mikakati yake ya kuhakikisha anamsajili mshambuliaji huyo huku uongozi wa klabu yake ukifanya mazungumzo na uongozi wa klabu ya Portsmouth .


Wakala wa Crouch amethibitisha kuwa mchezaji wake aliyefanikiwa kupachika mabao 16 katika michezo 49 akiwa The Pompey msimu uliopita yu sokoni.

No comments:

Post a Comment