
Klabu ya Manchester City imekubali kumsajili mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Argentina ambae pia alikuwa mtumishi kwenye vilabu vya West Ham Utd pamoja na Manchester United vyote vya nchini Uingereza Carlos Tevez.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amesajiliwa na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka mitano baada ya kupita kwenye vipimo vya afya usiku wa kuamkia leo.
Meneja wa klabu ya Man City boss Mark Hughes amesema hakika amefanikiwa kumnasa mchezaji alie kwenye kiwango cha juu cha kimataifa na ana imani Teves atakuwa suluhisho la kuisaidia klabu yake kwenye ushindani wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza.
Tevez, anatarajiwa kuonekana uwanjani akiwa amevaa jezi nambari 32 ambapo namba hiyo amekuwa akiitumia katika vilabu vya West Ham pamoja na Manchester United.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amesajiliwa na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka mitano baada ya kupita kwenye vipimo vya afya usiku wa kuamkia leo.
Meneja wa klabu ya Man City boss Mark Hughes amesema hakika amefanikiwa kumnasa mchezaji alie kwenye kiwango cha juu cha kimataifa na ana imani Teves atakuwa suluhisho la kuisaidia klabu yake kwenye ushindani wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza.
Tevez, anatarajiwa kuonekana uwanjani akiwa amevaa jezi nambari 32 ambapo namba hiyo amekuwa akiitumia katika vilabu vya West Ham pamoja na Manchester United.
No comments:
Post a Comment