KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Friday, November 20, 2009

FIFA YAONYESHA MSIMAMO.


Shirikisho la soka ulimwenguni kote FIFA limeyaweka kapuni maombi ya chama cha soka cha jamuhuri ya Ireland ya kutaka mchezo wa mtoano kati yao na Ufaransa urudiwe.

Ombi hilo la chama cha soka cha jamuhuri ya Ireland limewasilishwa jana baada kuzuka kwa utata wa maamuzi bao lililofungwa na William Gallas, ambae alipokea pasi kutoka kwa Thierry Henry alieunawa mpira mara mbili.

Chanzo cha habari toka ndani ya shirikisho la soka ulimwenguni kote FIFA kimeeleza kuwa hakuna njia yoyote ambayo itakubaliana na ombi la Jamuhuri ya Ireland hivyo matokeo yaliyopatikana katika mchezo wa jumatano yatasalia kama yalivyo.

No comments:

Post a Comment