
Wakala wa kiungo wa kimataifa toka nchini Italia na klabu ya AC Milan Gennaro Gattuso amekanusha taarifa za mchezaji wake kuwa mbioni kusajiliwa na klabu tajiri ya jijini Manchester inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Uingereza Manchester City.
Wakala wa kiungo huyo amekanusha taarifa hizo kufuatia kuwepo kwa uvumi ambao unadai kwamba kwa kipindi kirefu Gattuso hana furaha ya kuendenea kusalia huko San Siro hivyo yu radhi kuondoka katika ligi ya Sirie A na kujiunga na moja ya klabu inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Uingereza mwezi januari mwaka 2010.
No comments:
Post a Comment