KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Thursday, November 19, 2009

HENRY AZUA UTATA.


Beki wa timu ya taifa ya jamuhuri ya Ireland amelalamikia kitendo cha udanganyifu kilichofanywa na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ufaransa Thierry Henry cha kushika mpira mara mbili kabla ya kutoa pasi iliyozaa goli la kusawazisha lililofungwa William Gallas.

Dunne amesema Henry hakufanya kitendo cha uungwana cha kuunawa mpira na kushangilia mara baada ya bao kupatikana.

Beki huyo amesema pamoja na kusaka bao la kusawazisha ambalo lilikua likihitajika sana upande wa wapinzani wao bado Henry ambae anafahamika ulimwenguni kwa uwezo wake wa kucheza soka hakustahili kufanya kitendo hicho ambacho kimeonekana na wanasoka wote waliokuwa wakiufuatilia mchezo huo.

No comments:

Post a Comment