
Klabu ya Middlesbrough inayoshirikiu ligi daraja la kwana nchini Uingereza imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Stoke City Dave Kitson kwa mkopo wa miezi miwili.
kufuatia mafanikio hayo Kitson anakua mchezaji wa tatu kusajiliwa na Boro kwa mkopo tangu meneja Gordon Strachan alipochukua mikoba toka kwa Gareth Southgate.
Kitson huenda akacheza mechi yake ya kwanza mwishoni mwa juma hili hidi ya Nottingham Forest.
Wachezaji wengine waliosajiliwa klabuni hapo kwa mkopo ni pamoja na mshambuliaji Marcus Bent na kiungo Isaiah Osbourne.
Bent ameshapachika mabao mawili tu katika michezo 25 ya Ligi Kuu tangu alipojiunga na timu hiyo akitokea Reading mwaka 2008.
No comments:
Post a Comment