KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Tuesday, March 2, 2010

MAN UTD KUNANI?



Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza Manchester United wameshindwa kuitetea nafasi yao kimapato na kujikuta wakiteremshwa na klabu nguli za nchini Hispania msimu huu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa hii leo na kampuni inayoshughulika na uchunguzi wa mapato ya vilabu barani Ulaya iitwayo Deloitte Football Money imeonyesha kwamba Man utd wameshushwa katika orodha ya vilabu vilivyoingiza kiasi kikubwa cha cha mapato msimu uliopita ambapo nafasi ya kwanza imechukuliwa na klabu ya Real Madrid ikifuatiwa na Fc Barcelona.

Sababu kubwa iliyotolewa na kampuni hiyo juu ya kushushwa kwa Man Utd katika orodha hiyo ni deni la paund million 500 linaloikabili klabu hiyo inayomilikiwa na familia ya Glazer kutoka nchini Marekani.


Orodha kamili ya vilabu ni kama ifuatavyo.

1. Real Madrid 401.4 million euros

2. Barcelona 365.9m

3. Manchester United 327.0m

4. Bayern Munich 289.5m

5. Arsenal 263.0m

6. Chelsea 242.3m

8. Juventus 203.2m

7. Liverpool 217.0m

9. Internazionale 196.5m

10. AC Milan 196.5m

11. Hamburger SV 146.7m

12. Roma 146.4m

13. Lyon 139.6m

14. Marseille 133.2m

15. Tottenham Hotspur 132.7m

16. Schalke 124.5m

17. Werder Bremen 114.7m

18. Borussia Dortmund 103.5m

19. Manchester City 102.2m

20. Newcastle United 101.0m


No comments:

Post a Comment