KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Tuesday, March 2, 2010

SHUGHULI YAWA SHUGHULI !!!!!!

Familia ya Glazer inayoimiliki klabu ya Man Utd imetoa tamko la kutokua tayari kuiuza klabu hiyo na badala yake itaendelea kuimiliki kama utaratibu ulivyo hivi sasa.

Tamko la familia hiyo limetolewa baada ya malalamiko ya muda mrefu ya mashabiki wa klabu ya Man utd ambao wanaonekana kuchoshwa na utaratibu unaotumiwa na wamiliki hao ambao wanadai umekua ukiipa hasara klabu yao.


Msemaji wa familia hiyo amesema msimamo uliopo sasa kwa mabosi wake ni kuendelea kuiendesha klabu hiyo, na hawana mpango wowote wa kuiuza Man utd kwa mashabiki wake kama watakavyo na mashabiki hao.


Zogo la mashabiki wa klabu ya Man Utd la kutaka kuuziwa klabu yao, limeibuka kufuatia deni la paund million 500 ambalo lasemekana huenda likaigharimu kwa kiasi kikubwa klabu hiyo pale litakapolipwa.

No comments:

Post a Comment