KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, February 14, 2011

TORRES BADO HAJAONANA NA BOSI WAKE !


Mshambuliaji Fernando Torres amepasua ukweli kwa kueleza kwamba mpaka hii leo hajawahi kukutana na bosi wa ngazi ya juu wa klabu hiyo Roman Abramovich licha ya kusajiliwa kwa fedha nyingi akitokea Liverpool mwishoni mwa mwezi uliopita.

Torres amesema ukweli huo baada ya kuhojiwa na vyombo vya habari vya mjini London ambapo amebaisha kwamba ameshangazwa na hatua hiyo ambapo yeye binafsi alidhani huenda ingekua rahisi kuonana na kibopa huyo wa kirusi ambae ana hakika alifurahishwa na kukubali kwake kujiunga na The Blues.

Amesema licha ya kutokuwepo kwa mawasiliano kati yake na mkuu huyo bado anajihisi mwenye furaha na anaamini ipo siku atakutana nae na kubadilishana nae mawazo.

No comments:

Post a Comment