
Sir Alex Ferguson amesema msimamo wa meneja huyo kutoka nchini Italia unaonyesha ni vipi alivyo na maamuzi yenye nguvu ndani ya klabu ya Man City ambayo ana hakika haimtazami yoyote yule klabuni hapo kwa uwezo ama umaarufu alionao.
Amesema mchezaji siku zote anastahili kutii amri anayoamrishwa na mkuu wake wa kazi na yeye binafsi hakufurahishwa na kitendo alichokionyesha mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka, 27 ambae pia aliwahi kuwa chini yake huko Old Trafford.

Paul Scholes amesema anamuelewa vizuri Carlos Tevez na kikubwa alichonacho katika tabia ni kuhitaji kucheza kila mara na linapojitokeza jambo kinyume na hilo hukasirishwa na hatua hiyo.
Amesema yeye binafsi anakumbuka mwaka 2001, aliwahi kugoma kutii amri ya Sir Alex Ferguson ambae alimtaka kuingia uwanjani kama mchezaji wa akiba katika mchezo wa kuwania kombe la ligi na matokeo yake alitupwa benchi katika mchezo dhidi ya Liverpool.

Taarifa hiyo imetoka huko jijini London huku viongozi wa Man City wakiendelea kutafakari hatua za kumchukulia mshambuliaji huyo baada ya kumsimamisha kwa majuma mawili na pengine huenda adhabu hiyo ikaongezwa baada ya kufanyika kwa uchunguzi.
Hata hivyo kuna taarifa kwamba wabeba nyundo hao wa London wapo tayari kumlipa Carols Teves mshahara wa paundi 250,000 kwa juma kwa muda wa miezi mitatu, mshahara ambao anaupata kwa sasa huko Etihad Stadium.

Wakati hayo yakijiri mshambuliaji mwingine wa Manchester City Edin Dzeko amemuomba radhi Roberto Mancini kufuatia kitendo cha utovu wa nidhamu alichokionyesha baada ya kutolewa nje katika mchezo dhidi ya Fc Bayern Munich na nafasi yake kuchukuliwa na Nigel De Jong.
Edin Dzeko amesema hakudhamiria kufanya kitendo cha kutupa, Track Sout bali alifanya hivyo baada ya kushindwa kutimiza malengo ya kuisaidia klabu yake ambayo tayari ilikua nyuma kwa idadi ya mabao mawili kwa sifuri.
No comments:
Post a Comment