
Thomas DiBenedetto anakuwa raisi wa 22 wa klabu hiyo ya mjini Roma, na sasa anaichukua kutoka mikononi mwa familia ya Sensi ambayo imekuwa madarakani kwa muda wa miaka 18 iliyopita.
Hatua za kutangazwa kwa mfanyabiashara huyo zimethibitishwa muda mchache baada ya masuala la kisheria kukamilishwa na mwanasheria wa benki UniCredit Roberto Cappelli ambae alipitia mipango yote ya kisheria na kuona haina doa kwa Thomas DiBenedetto.
Utaratibu wa kuthibitishwa na mwanasheria wa benki UniCredit, umekuja kufuatia Thomas DiBenedetto, kufanya kazi na benki hiyo kwa kipindi kirefu hatua ambayo ilipelekea kufanya mpango wa kuinunua AS Roma kwa uaminifu uliopo dhidi ya benki hiyo.
Kwa mantiki hiyo sasa Thomas DiBenedetto anakuwa raisi wa kwanza wa klabu ya AS Roma ambae si raia wa nchini italia pamoja na kuwa mmiliki wa klabu ya michezo katika ardhi ya nchi hiyo.
No comments:
Post a Comment