KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, September 28, 2011

Titus Bramble ASHIKWA NA POLISI UINGEREZA.

Beki wa klabu ya Sunderland Titus Bramble anashikiliwa na jeshi la polisi nchini uingereza kufuatia kukabiliwa na tuhuma za unyanyasaji wa kijinsia sambamba na tuhuma za dawa za kulevya.

Taarifa iliyotolewa na jeshi hilo zimeeleza kwamba beki huyo mwenye umri wa miaka 30 alikamatwa mapema hii leo na amefanyiwa mahojiano yanayohusianana tuhuma zinazomkabnili.

Titus Bramble anatuhumiwa kufanya vitendo hivyo usiku wa kuamkia hii leo hatua ambayo imewashangaza wengi kutokana na muonekano wake anapokua uwanjani.

Beki huyo alikua miongoni mwa wachezaji wa Sunderland waliocheza mchezo wa ligi kuu ya nchini Uingereza siku mbili zilizopita huko carrow road dhidi ya wenyeji Norwich city walioibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja.

Titus Bramble alianza kutambulika katika medani ya soka mara baada ya kupandishwa katika kikosi cha kwanza cha Ipswich town na baada ya hapo alisajiliwa na klabu ya Newcastel Utd kwa ada ya uhamisho wa paund million 5 mwaka 2002.

Alikaa huko St James Park kwa kipindi cha miaka mitano kabl ya kuihama Newcastle na kujiunga na Wigan mnamo mwaka 2007 na kisha aliachana na klabu hiyo baada ya kusajiliwa na Sunderland mwanzoni mwa msimu uliopita.

Mwezi uliopita mdogo wa Titus Bramble aitwae Tesfaye Bramble alihukumiwa kifungo cha miaka minne na nusu baada ya kukutwa na hatia ya kubaka.

Tesfaye Bramble mwenye umri wa miaka 19, hakupata nafasiya kufahamika vyema katika medani ya soka, kufuatia kucheza ligi za chini za nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment