KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, September 28, 2011

Carlos Tevez ATOA KALI YA MWAKA MAN CITY.


Mshambuliaji kutoka nchini Argentina Carlos Tevez, ameibua zogo jipya huko Etihad Stadium baada ya kukataa kutumika kama mchezaji wa akiba katika mchezo wa kundi la dhidi ya FC Bayern Munich waliokua nyumbani Allianze Arena.

Hatua hiyo imeonekana kummkera mno meneja wa Man city Roberto Mancini ambapo amesema hatompa mshambuliaji huyo nafasi nyingine ya kucheza katika kikosi chake hadi hapo muda wa kuondoka Etihad Stadium utakapotimia.

Amesema hakufurahishwa na kitendo hicho cha Carlos Tevez ambae tayari alikua ameshamueleza taarifa za kumtumia kama mchezaji wa akiba lakini alipomuamuru ajiandae alimkatalia kata kata huku zikiwa zimesalia dakika 34 mpambano kumalizika.

Kufuatia hatua hiyo Roberto Mancini amedai kwamba kila mmoja anastahili kumuheshimu mwingine klabuni hapo kutokana na nafasi aliyonayo na sasa haoni sababu ya kuendelea kumtumia Tevez kama mchezaji ambae anartegemewa kikosini.

Kwa upande wa Carlos Tevez mwenye umri wa miaka 27, amejitetea kwa kusema hakukataa kucheza katika mchezo huo wa jana na msimamo wake ulichukuliwa tofauti na meneja huyo kutoka nchini Italia.

Carlos Tevez pia amewataka radhi mashabiki wa Man city kwa kile kilichoonekana usiku wa kuamkia hii leo, huku akieleza wazi kwamba bado anaipenda klabu hiyo na atakua tayari kufanya atakachoelekezwa.

Hii si mara ya kwanza kwa wawili hao kusigana, kwani kama itakumbukwa vyema tayari Carlos Teves ameshawahi kukwaruzana mara kwa mara na Roberto Mancini na kufikia hatua mshambuliaji huyo kutaka kuondoka na kurejea nyumbani kwao Argentina kwa kisingizio cha kuhitaji kuwa karibu na familia yake yenye watoto wawili wa kike.

Katika mchezo huo wa kundi la kwanza wenyeji FC Bayern Munich walitimiza malengo yao ya kupata ushindi nyumbani, baada ya kuwabanjua wageni wao mabao mawili kwa sifuri yaliyofungwa na Mario Gomez katika dakika ya 38 na 45.

No comments:

Post a Comment