
Kiungo wa kimataifa toka nchini Uingereza na klabu ya Chelsea Frank Lampard amesema anaamini rafiki yake wa karibu John Terry ataendelea kusalia Chelsea na kuzitupilia mbali taratibu za kujiunga na klabu ya Manchester City.
Lampard amesema nahodha huyo wa klabu ya Chelsea bado ana mapenzi ya dhati na klabu yake ya sasa hivyo itamuuwia vigumu kuianza safari ya kuondoka Stamford Bridge na kuelekea City Of Machester.
Amesema pamoja na kuwepo kwa kila aina ya mvuto ambao unatolewea na uongozi wa klabu ya ManCity bado anaamini Terry hatovutiwa na hali hiyo.
Lampard, ambae alikaribia kujiunga na klabu ya Inter Milan inayofundishwa na meneja wa zamani wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho msimu uliopita, ameongeza kuwa haoni sababu ya John Terry kuondoka kwenye klabu ya Chelsea ambayo ina mafanikio makubwa mbali na klabu inayomuhitaji kwa sasa.
Hivi karibuni klabu ya Man City iliripotiwa kuwa tayari kumlipa John Terry paund lakini mbili kama mashahara wake kwa juma, iwapo atakubalia kujiunga na klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment