
Kiungo wa kimataifa toka nchini Ufaransa na klabu hiyo ya Arsenal Samir Nasri atakuwa nje ya uwanja kwa muda kufuatia kuvunjika mguu alipokuwa mazoezini hii leo.
Nasri ambae ni mmoja wa wachezaji wa Arsenal walioweka kambi na huko nchini Austria kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza huenda akawa nje ya uwanja wa muda wa miezi miwili ama mitatu, kwa mujibu wa madaktari wa klabu hiyo.
Kufuatia gharka hiyo kiungo huyo natarajia kukosa sehemu ya mwanzo wa msimu wa ligi kuu pamoja na baadhi ya michezo ya timu yake ya taifa ya Ufaransa ambayo inawania nafasi ya kufuzu kucheza kombe la duniani mwaka 2010.
No comments:
Post a Comment