
Kipa wa klabu ya Tottenham Carlo Cudicini anaendelea vyema na ameonyesha dalili nzuri za kupona majeraha yake aliyoyapata kwenye ajali kati kati ya juma lililopita.
Kipa huyo pamoja na kuonyesha dalili njema za kupona itamlazimu kuwa nje ya uwanja wa muda wa majuma 12 ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.
Carlo Cudicini mwenye umri wa miaka 36 alipata ajali baada ya pikipiki yake aina ya BMW kugongana na gari aina ya Ford Fiesta ambalo lilikua likiendeshwa mwana mama.
No comments:
Post a Comment