KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Sunday, November 15, 2009

AJALI + Carlo Cudicini = MAJUMA 12


Kipa wa klabu ya Tottenham Carlo Cudicini anaendelea vyema na ameonyesha dalili nzuri za kupona majeraha yake aliyoyapata kwenye ajali kati kati ya juma lililopita.


Kipa huyo pamoja na kuonyesha dalili njema za kupona itamlazimu kuwa nje ya uwanja wa muda wa majuma 12 ili aweze kurejea katika hali yake ya kawaida.


Carlo Cudicini mwenye umri wa miaka 36 alipata ajali baada ya pikipiki yake aina ya BMW kugongana na gari aina ya Ford Fiesta ambalo lilikua likiendeshwa mwana mama.

No comments:

Post a Comment