Maelfu ya watu wamehudhuria ibada ya aliekuwa kipa wa timu ya taifa ya Ujerumani pamoja na klabu ya Hannover 96, Robert Enke aliefariki kati kati ya juma hili.Ibada hiyo imefanyika katika uwanja wa mpira uliopo kaskazini wa Hanover.
Wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa waliongoza katika kutoa risala za kumkumbuka ya kipa huyo ambae alifikwa na umauti baada ya kugongwa na treni hali mbayo iliwashangaza wengi nchini Ujerumani pamoja na duniani kote.
Mke wa marehemu ameeleza kwamba Enke aliishi kwa muda mrefu katika hali ya unyonge, kabla ya kuamua kujirusha mbele ya treni iliyokuwa katika mwendo wa kasi.

No comments:
Post a Comment