
Benchi la ufundi la klabu ya Liverpool limeonyesha kuwa tayari kumsajili mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Croatia na klabu ya Arsenal Eduardo da Silva.
Liverpool wameonyesha hatua hiyo kufuatia taarifa zinazodai kwamba mshambuliaji huyo kwa sasa hana raha huko Ashburton Grove kufuatia hatua finyu zinazo onekana za kutopewa mkataba mpya na klabu yake ya Arsenal.
Meneja wa klabu ya Liverpool Rafa Benitez tayari ameshaandaa kitita cha paund million 10 ambacho kitatumika kama ada ya uhamisho wa Eduardo ambae huenda kapewa nafasi ya kusaidiana na David Ngog, katika safu ya ushambuliaji ya klabu hiyo.
No comments:
Post a Comment