
Kufuatia kichapo cha mabao matatu kwa sifuri, meneja wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger amesema kuna ulazima mkubwa wa kuanza kufikiria upya suala la kufanya usajili kwenye dirisha dogo la usajili mwezi januari mwaka 2010.
Wenger amelizungumza suala hilo baada ya kuulizwa maswali na waandishi wa habari mara baada ya mchezo wa jana ambapo amesema kiukweli kikosi chake kinahitaji usaidizi mkubwa baada ya kuumia kwa mshambuliaji wake Robin Van Parsie.
No comments:
Post a Comment