
Hofu imetanda kwa mashabiki wa klabu ya Arsenal kufuatia mshambuliaji wao tegemezi kwa sasa Robin van Persie kuumia kwenye mchezo wa jana wa kimataifa wa kirafiki kati ya timu yake ya taifa ya Uholanzi dhidi ya timu ya taifa ya Italia.
Mshambuliaji huyo ameumizwa kifundo cha mguu na yasemekana huenda akawa nje ya uwanja kwa zaidi ya siku thelathini hilo limethibitishwa na kocha wa timu ya taifa ya Uholanzi Bert van Marwijk.
Kufuatia hali hiyo ndoto za Van Parsie kucheza mchezo wa kombe la ligi dhidi ya Man City inapotea na itamlazimu kuwa mtazamaji wa timu ya vijana ya Arsenal ambayo inatarajiwa kucheza kwenye pambano hilo la Disemba mosi.
No comments:
Post a Comment