KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, November 16, 2009

George Burley KIKAANGONI.


Kamati ya utendaji ya chama cha soka nchini Scotland *Scottish Football Association* inatarajia kukutana na kujadili mustakabali wa kocha mkuu wa timu ya taifa ya nchi hiyo George Burley.


Kikao hicho kinatarajiwa kutoa jibu sahihi kwa kocha huyo kama ataendelea kubaki na kazi yake ama la, hasa baada ya timu ya taifa ya Scotland kukosa nafasi ya kushiriki fainali za kombe la dunia za mwaka 2010.


Burley alionekana kushindwa kuipeleka kwenye hatua ya mchezo wa mtoano timu ya taifa ya Scotland baada ya kukubali kichapo cha mabao matatu kwa sifuri toka kwa timu ya taifa ya Wales.

No comments:

Post a Comment