KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, November 16, 2009

NGOMA YAPELEKWA SUDAN.


Baada ya kufanya kweli kwa ushindi wa mabao mawili kwa sifuri mwishoni mwa juma lililopita timu ya taifa ya Misri inatarajia kucheza mchezo wa mtoano nchini Sudan dhidi ya timu ya Algeria kwenye mchezo wa kuwani nafasi ya kushiriki fainali za kombe la dunia mwaka 2010.

Mchezo huo utakaochezwa katika uwanja huru unatarajiwa kupigwa siku ya jumatano hatua ambayo itawalazimu na mashabiki wa nchi hizo kusogea huko nchini Sudan kuzishangilia timu zao.

Kufuatia ushindi wa mabao mawili kwa sifuri walioupata Misri ulizifanya timu hizo kuwa sawa katika kila hali hatua ambayo imelilazimu shirikisho la soka duniani FIFA kuamuru mchezo huo uchezwe kwenye uwanja huru ili kumpata yule atakaelekea bondeni mwa bara la Afrika mwaka 2010.

No comments:

Post a Comment