
Mshambuliaji nyota wa kimataifa toka nchini Nigeria Stephen Worgu anayecheza soka la kulipwa nchini Sudan amekuhumiwa kuchapwa viboko na kulipa fainai baada ya kukutwa na hatia ya kunywa pombe na kuendesha gari.
Worgu ambaye anaichezea klabu ya Al Merreikh amekutwa na kosa hilo ambalo ni kubwa huko kaskazini ya Sudan tofauti na ilivyo huko Kusini mwa Sudan ambapo waumini wa dini ya Kiislam ni wachache.
Hata hivyo adhabu hiyo bado haijatekelezwa kufuatia wakili wa mchezaji huyo kukata rufaa iwapo atashindwa rufaa hiyo Worgu atatakiwa kuchapwa viboko 40 na kulipa faini ya paundi za Sudan 250 sawa na dola 100 za Marekani .
Paundi 50 itakuwa ni kwa ajili ya kunywa pombe na paundi 200 kwa ajili ya kuendesha gari akiwa amelewa.
Itakumbukwa kwamba Worgu alisajiliwa na klabu ya Al Merreikh kwa uhamisho wa ada ya dola za kimarekani milioni 2.6 akitokea katika klabu ya Enyimba ya Nigeria,uhamisho ambao ni wa ghali katika historia barani Afrika .
Worgu alikuwa mfungaji bora katika ligi ya klabu bingwa barani Afrika mwaka 2008 kwa kufunga mabao 13 lakini tangu alipohamia nchini Sudan kiwango chake kimeshuka.
Worgu ambaye anaichezea klabu ya Al Merreikh amekutwa na kosa hilo ambalo ni kubwa huko kaskazini ya Sudan tofauti na ilivyo huko Kusini mwa Sudan ambapo waumini wa dini ya Kiislam ni wachache.
Hata hivyo adhabu hiyo bado haijatekelezwa kufuatia wakili wa mchezaji huyo kukata rufaa iwapo atashindwa rufaa hiyo Worgu atatakiwa kuchapwa viboko 40 na kulipa faini ya paundi za Sudan 250 sawa na dola 100 za Marekani .
Paundi 50 itakuwa ni kwa ajili ya kunywa pombe na paundi 200 kwa ajili ya kuendesha gari akiwa amelewa.
Itakumbukwa kwamba Worgu alisajiliwa na klabu ya Al Merreikh kwa uhamisho wa ada ya dola za kimarekani milioni 2.6 akitokea katika klabu ya Enyimba ya Nigeria,uhamisho ambao ni wa ghali katika historia barani Afrika .
Worgu alikuwa mfungaji bora katika ligi ya klabu bingwa barani Afrika mwaka 2008 kwa kufunga mabao 13 lakini tangu alipohamia nchini Sudan kiwango chake kimeshuka.
No comments:
Post a Comment