KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Sunday, November 15, 2009

NI KWELI ATAREJEA?


Aliyekua meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amekiri kwamba huenda akarejea nchini uingereza kufanya kazi na pengine akamiliza muda wake wa kufundisha soka akiwa nchini humo .

Mourinho ambaye kwa sasa ni meneja wa klabu ya Inter Milan, kwa muda sasa amewakosesha raha mashabiki wa soka nchini Uingereza kutokana na msimamo wake na mafanikio aliyoyapata baada ya kuwasili Stamford Bridge mwezi September 2007 akishinda mataji mawili mfululizo ya ligi ya Premier na kombe la FA Cup na mataji mawili ya Carling.


Mourhino aliweza kujizolea mashabiki wengi kwa muda wa miaka mitatu na nusu aliyokaa nchini Uingereza na baada ya kuhamia nchini Italia ameendeleza mafanikio yake kwa kushinda taji la Scudeto katika ligi kuu ya soka nchini Italia maarufu kama Serie A.


Taarifa zinaeleza kuwa huenda Mourinho akachukua nafasi ya Sir Alex Ferguson atakapostaafu kuifundisha klabu ya Manchester United.

No comments:

Post a Comment