
Beki wa kulia wa klabu ya Chelsea Jose Bosingwa ataendelea kusalia kwenye benchi la wachezaji majetruhi wa klabu hiyo kufuatia maumivu yake ya goti kuchelewa kupona ndani ya muda uliokuwa umekusudiwa.
Beki huyo wa kimataifa toka nchini Ureno pia huenda akazikosa fainali za kombe la dunia za mwaka huu zitakazounguruma huko nchini Afrika kusini kufuatia kuhitaji kufanyiwa upasuaji mwingine ambao utamfanya arejee tena uwanjani katika kipindi cha maandalizi ya msimu ujao.
No comments:
Post a Comment