KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Tuesday, March 2, 2010

BUNDI AENDELEA KUTUAMA ANFIELD.



Wakawa katika wakati wa kutaka kurejea katika harakati za kucheza ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao kwa kuhakikisha angalau wanamaliza msimu wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza kwa kuikamata nafasi ya nne, majogoo wa jiji Liverpool wameendelea kukumbwa na mikasa kufuatia beki wao wa kimataifa toka nchini Slovakia Martin Skrtel kuthibitika hatocheza kwa kipindi cha msimu kilichosalia.


Skrtel hatocheza katika kipindi cha msimu kilichosalia baada ya vipimo kuonyesha amevunjika mfupa wa mguu *Metatarsal* kwenye mchezo wa ligi ya Europa uliopigwa kati kati ya juma lililopita dhidi ya mabingwa wa soka nchini Romania Unirea Urziceni ambapo Liverpool walichomoza na ushindi wa mabao matatu kwa moja.


Meneja wa klabu ya Liverpool Rafael Benitez amesema beki huyo mwenye umri wa miaka 25, hatoahitaji kufanyiwa upasuaji kwa sasa, hivyo atalazimika kufanyiwa hivyo mwishoni mwa mwezi wa nne.

No comments:

Post a Comment