KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Thursday, March 4, 2010

CAPELLO AWAPA 5 MASHABIKI.



Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uingereza Fabio amewashukuru sana mashabiki waliohudhuria kushuhudia mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa jana kati ya vijana wake dhidi ya mabingwa wa soka toka barani afrika Misri.


Shukurani hizo za Capello zimekuja baada ya mashabiki hao kutoonyesha vitendo vya kuwa kinyume na aliekua nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza John Terry ambae yupo kwenye skendo ya kutembea na rafiki wa zamani wa Wyne Bridge.


Mara baada ya mchezo huo wa kimataifa wa kirafiki kumalizika kwenye uwanja wa Emirates Capello alionekana kufurahishwa na na hatua ya mashabiki hao ambapo ilimlazimu kutoa shukurani zake za dhati kwa kuwaelezea kuwa walionyesha ujasiri mkubwa wa kuwa pamoja na John Terry.

No comments:

Post a Comment