KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Saturday, March 13, 2010

MANCINI ASITISHA MAZUNGUMZO.


Katika kuhakikisha wachezaji wake wanaelekeza mawazo yao katika ushindani unaowakabili kwa sasa, meneja wa klabu ya Manchester City Roberto Mancin amesitisha mazungumzo ya kumsainisha mkataba mpya winga wake wa kimataifa toka nchini Uingereza Shaun Wright-Phillips.


Akitetea uamuzi wake Mancin alieichukua Man City kutoka kwa Mark Hughes alietimuliwa kazi mwezi Disemba mwaka jana, amesema kwa wakati huu haoni kama kuna manufaa sana kwake na wachezaji wake kwa ujumla kufanya mazungumzo ya mikataba ili hali wanakabiliwa na ushindani wa kuiwania nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment