
Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema kesho huenda akamchezesha nahodha wa kikosi chake Cesc Fabregas kwenye mchezo wa pili wa hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Fc Porto.
Wenger anatazamia kumchezesha kiungo huyo wa kimataifa toka nchini Hispania huku kukiwepo na taarifa zilizoeleza kwamba Fabrigas anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja ambayo aliyapata kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza uliochezwa mwishoni mwa juma lililopita.
No comments:
Post a Comment