KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, May 26, 2010

FRAN MERIDA AREJEA NYUMBANI.


Kiungo wa kimataifa toka nchini Hispania Fran Merida amekamilisha utaratibu wa kujiunga na klabu ya Atletico Madrid akitokea kwenye klabu ya Arsenal ya nchini Uingereza.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 amekamilisha utaratibu huo kufuatia mkataba wake na klabu ya Arsenal kufikia kikomo hivyo imemlazimu kuhama akiwa kama mchezaji huru.

Sababu kubwa iliyomuhamisha kiungo huyo ni kufuatia kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha klabu ya Arsenal.

Itakumbukwa kuwa Merida akiujiunga na klabu ya arsenal mwaka 2006 akitokea FC Barcelona.

No comments:

Post a Comment