
Mshambuliaji wa klabu ya Middlesbrough ya nchini Uingereza Scott McDonald amekua miongoni mwa wachezaji watatu waliachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Australia kitakachoshiriki fainali za kombe la dunia.
Mshambuliaji huyo ameachwa na kocha mkuu wa timu hiyo Pim Verbeek baada ya kuonyesha kiwango duni kwenye mchezo wa jana wa kujipima ubavu dhidi ya New Zealand ambao walikubali kibano cha mabao mawili kwa moja.
Mshambuliaji huyo ameachwa na kocha mkuu wa timu hiyo Pim Verbeek baada ya kuonyesha kiwango duni kwenye mchezo wa jana wa kujipima ubavu dhidi ya New Zealand ambao walikubali kibano cha mabao mawili kwa moja.
Sababu nyingine iliyomuondoa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 kikosini ni kufuatia kukosa kupachika bao hata moja kwenye michezo 16 ya timu ya taifa aliyocheza.
Kuondolewa kwa mchezaji huyo kunamaanisha timu ya taifa ya Australia imesaliwa na washambuliajni watatu ambao ni Josh Kennedy, Harry Kewell pamoja na Nikita Rukavysya.
Wachezaji wengine aliotemwa na Pim Verbeek ni kiungo wa klabu ya Crystal Palace Nick Carle pamoja na beki Jade North .
Kuondolewa kwa mchezaji huyo kunamaanisha timu ya taifa ya Australia imesaliwa na washambuliajni watatu ambao ni Josh Kennedy, Harry Kewell pamoja na Nikita Rukavysya.
Wachezaji wengine aliotemwa na Pim Verbeek ni kiungo wa klabu ya Crystal Palace Nick Carle pamoja na beki Jade North .
No comments:
Post a Comment