Meneja wa klabu ya Man Utd Sir Alex Ferguson amezionya klabu zinazotumia fedha kwa fujo kwa lengo la kufanya usajili wa wachezaji huku akizieleza katu ubingwa haunuliwi kwa fedha.
Sir Alex Ferguson ametoa onyo hilo, baada ya kuonekana kuchukizwa na hatua ya matumizi mabaya ya fedha yanayofanywa na wapinzani wake katika mji wa Manchester nchini Uingereza Man City ambao tayari wameshatumia zaidi ya paund million 150.
Mzee huyo toka nchini Scotland amesema klabu hizo zinatakiwa kufahamu suala la kutwaa ubingwa si la kutumia fedha nyingi kwa wakati mmoja bali ni suala la kujiandaa kwa muda mrefu hadi kufikia hatua ya kuwa na kikosi bora.
No comments:
Post a Comment