KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, August 25, 2010

NDOTO ZA UTURUKI ZAFIKIA MWISHO.


Mshambuliaji wa kimataifa toka nchini Brazil Róbson de Souza Robinho amefuta ndoto zake za kujiunga na klabu ya Fenerbahce ya nchini Uturuki na badala yake anataka kujiunga na moja ya klabu za nchini Italia ama Hispania.

Róbson de Souza Robinho ametoa msimamo huo ikiwa ni siku chache zimepita baada ya meneja wa klabu ya Man City Roberto Mancini kuahidi kulifanyia kazi suala la mchezaji huyo anaetaka kuondona City Of Manchester.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 amesema alitamani sana kuelekea nchini Uturuki baada ya uongozi wa klabu ya Fenerbahce kutuma ofa ya kutaka kumsajili lakini, ameonea ni bora arejee Hispania ama kuelekea nchini Italia.

Hata hivyo bado kuna shaka juu ya usajili wa mchezaji huyo kwa kuhofia huenda akashindwa kuuwahi muda wa usajili unaofikia kikomo August 31 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment