KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Wednesday, November 24, 2010

AL-AHLY WAMTANGAZA KOCHA MPYA.


Klabu ya Al Ahly ya nchini Misri imemtangaza mchezaji wa zamani wa klabu hiyo Abdel Aziz Abdel Shafi kuwa kocha wa muda wa klabu hiyo.

Uongozi wa klabu hiyo umemteua Abdel Aziz Abdel Shafi kuwa kocha wa muda kufuatia aliekua kocha klabuni hapo Hossam Al Badry, kutangaza kujiuzulu mwishoni mwa juma lililopita baada ya kukubalia kisago kutoka kwa Ismailia katika mchezo wa ligi.

Shafi ameteuliwa kushika nafasi hiyo ambapo atasaidiana na Sayed Abdel Hafeez, ambae anatarajiwa kuwa mkurugenzi wa mfundi wa chama cha soka nchini Misri.

No comments:

Post a Comment