KARIBU KWENYE BLOGU YA XTRA COVER ILI UWEZE KUFAHAMU YALE YANAYOTOKEA NJE YA MIPAKA YA NCHI YETU, PIA WAWEZA KUTOA MAONI YAKO KWA TAARIFA YOYOTE ITAKAYO KUKUNA.

Monday, July 11, 2011

MANA UTD KUCHEZA DHIDI YA AKINA BECKHAM.





Kiungo mwenye nyota ya kupendwa ulimwenguni David Beckham, anajiandaa kucheza na kikosi cha klabu yake ya zamani ya Man utd ambacho kitafanya ziara nchini humo tayari kwa maandalizi ya msimu mpya wa ligi.


David Beckham, anajiandaa kucheza mchezo huo, baada ya kuchaguliwa na kuwa miongoni mwa wachezaji 11 wanaounda kikosi cha Major League football All-Star ambacho kitashuka dimbani July 27 kupambana na mabingwa hao wa Uongereza kwenye uwanja wa Red Bull Arena uliopo mjini New Jersey.
Hata hivyo hii itakua si mara ya kwanza kwa Beckham, kucheza na kikosi cha Man utd kwani alishafanya hivyo mwezi May, katika mchezo maalum uliokua na lengo la kumuaga nahodha na beki wa zamani wa klabu hiyo ya mjini Manchester Gary Neville.


Katika kikosi hicho kinachoundwa na wachezaji waneocheza ligi kuu ya nchini Marekani pia yupo kiungo mshambuliaji ambae aliwahi kuichezea Everton kwa mkopo Landon Donovan, beki wa zamani wa FC Barcelona Rafael Marquez pamoja na mshambuliaji wa zamani wa klbu ya Arsenal pamoja na Barcelona Thierry Henry.

No comments:

Post a Comment