




Sir Alex Ferguson alitumia maneno hayo kwa kuwalaumu wachezaji wake ambao walionyesha uwezo mkubwa katika kipindi cha kwanza ambacho kilishuhudia wakielekea mapumziko huku wakiongoza mabao mawili kwa sifuri lakini hali iliwabadilikia katika kipindi cha pili.
Amesema endapo wachezaji wake wangekuwa makini na kulinda mabao mawili yaliyopatikana katika kipindi cha kwanza kulikua na ulazima wa kuongeza bao lingine na pengine kupata point tatu muhimu ambazo zingewapa nafasi ya kukaa pazuri katika msimamo wa kundi la tatu.
Nae meneja wa Fc Basle Thorsten Fink amepasua ukweli wa kile kilichopelekea wachezaji wake kuonyesha juhudi na kufanikia kurejea katika mchezo na mwishowe kulazimishwa sare ya mabao matatu kwa matatu.
Thorsten Fink amesema kutokukata tamaa na mabao waliyofungwa katika kipindi cha kwanza ilikuwa ni sera yao na aliwaeleza suala hilo wachezaji wake wakati wa mapumziko.
Hata hivyo amedai kwamba walijiandaa vyema kabla ya mpambano huo wa jana ambapo alijua wanakwenda kupambana na timu nzuri na yenye kujua kulikabili lango la wapinzani.
No comments:
Post a Comment