
Uongozi wa klabu hiyo ya Etihad Stadium umefikia maamuzi hayo baada ya kupoa taarifa kamili kutoka kwa meneja Roberto Mancini ambae alikiri kuchukizwa na tabia aliyoonyeshwa na mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27.
Taarifa iliyotolewa imeeleza kwamba kwa kipindi cha majuma mawili, uchunguzi utafanyika wa kubaini nini chanzo kilichopelekea Caros Tevez kugoma kuingia uwanjani kama mchezaji wa akiba wakati tayari Bayern Munich walikua wanaongoza mabao mawili kwa sifuri yaliyofungwa na Mario Gomes.
Taarifa hio imeongeza kwamba Carlos Tevez akiwa anaendelea na adhabu hiyo hatoruhusiwa kufanya shughuli yoyote klabuni hapo pamoja na kujumuika na wachezaji wenzake watakapokua mazoezini.

Kama itakumbukwa vyema Carlos Tevez alitoa kauli yake mara baada ya kurejea nchini Uingereza wakitokea nchini Ujerumania mbapo alisema kuwa benchi la ufundi lilimuelewa vibaya kufuatia maamuzi aliyoyafanya, lakini akaahidi atakuwa tayari kufanya chochote atakachoagizwa kukifanya klabuni hapo.
No comments:
Post a Comment